Sunday, November 3, 2013

UPANGAJI WA VIWANGO VYA ALAMA, MATUMIZI YA ALAMA ENDELEVU YA MWANAFUNZI NA UFAULU.(MABADILIKO YA VIWANGO VIPYA VYA UFAULU "new grades")

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
UPANGAJI WA VIWANGO VYA ALAMA, MATUMIZI YA ALAMA ENDELEVU YA MWANAFUNZI NA UFAULU
1. UTANGULIZI
Wizara imekusanya maoni ya Wadau wa Elimu kuhusu Upangaji wa Viwango vya Alama (Grade Ranges) katika Mitihani ya Kuhitimu Kidato cha Nne na cha Sita pamoja na Matumizi ya Alama za Tathmini Endelevu ya Mwanafunzi (Continuous Assessment ama CA) kwa ajili ya kuamua kiwango cha ufaulu wa mwanafunzi. Maoni ya wadau yamekusanywa kwa sababu kwa muda mrefu sasa upangaji wa viwango vya alama vinavyotumika na utaratibu wake katika mitihani ya kuhitimu Kidato cha Nne na Kidato cha Sita umekuwa haufanani pamoja na kwamba mitihani hiyo yote ni ya elimu ya sekondari. Pia mfumo masuala mbalimbali ya mitihani katika elimu ya sekondari umekuwa na miundo tofauti ikiwemo ule unaotumika shuleni na ule wa Baraza la Mitihani la Taifa. Kwa sasa kuna miundo mikuu miwili katika mfumo huo. Muundo wa Kwanza ni upangaji wa viwango katika ngazi ya Shule ambapo Alama Mgando (Fixed Grade Ranges) zifuatazo hutumika kupanga madaraja: A = 81 每 100; B = 61 每 80; C = 41 每 60; D = 21 每 40 na F = 0 每 20. Muundo huu umetumika kwa muda mrefu na umezoeleka kwa walimu na wanafunzi wa elimu ya sekondari kwa ujumla. Muundo wa Pili ni wa viwango vinavyotumiwa na Baraza la Mitihani la Taifa ambapo ambapo kabla ya mwaka 2012 muundo wa viwango nyumbufu (flexible grade ranges) ulitumika. Katika muundo huu uwigo wa alama ulibadilika badilika kulingana na hali ya matokeo ilivyokuwa kwa mwaka husika. Lakini kuanzia mwaka 2012, Serikali iliamua kutumia mfumo wa Upangaji wa Alama Mgando (Fixed Grade Range) kwa Kidato cha Nne na Kidato cha Sita. Katika mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2012 Baraza lilitumia mfumo huu wa alama mgando ambapo: A = 80 每 100, B = 65 每 79, C = 50 每 64, D = 35 每 49, F = 0 每 34. Kwa upande wa Kidato cha Sita Baraza lilitumia mfumo wa A = 80 每 100; B = 75 - 79; C = 65 每 74; D = 55 每 64; E = 45 每 54; S = 40 每 44 na F = 0 每 39. Mifumo hii ya Baraza haikuwa inafahamika kwa wadau na hivyo kuwa sehemu ya malalamiko katika sekta ya elimu na mafunzo. Vilevile, Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 1995 imeelekeza kwamba katika kuamua kiwango cha ufaulu wa mwanafunzi wa elimu ya sekondari, Alama za CA zitachangia asilimia hamsini (50%) na Mtihani wa mwisho utachangia asilimia hamsini (50%). Kwa upande wa Zanzibar, CA zimekuwa zikiandaliwa kwa mfumo wa asilimia arobaini (40%) na mtihani wa mwisho asilimia sitini (60%). Pamoja na kwamba Baraza halijawahi kuutumia mifumo hii tangu ilipowekwa, kumekuwa na mitazamo, maoni na mapendekezo tofauti katika muundo na matumizi ya alama za CA. Kuna mawazo pia kwamba mfumo wa CA kuchangia matokeo ya mwisho ya mwanafunzi pia utumike kwa watahiniwa wa kujitegemea (private candidates). Kwa sasa matokeo ya mitihani ya watahiniwa hawa yamekuwa yakitumia alama za mtihani wa mwisho tu na hivyo kutafsiriwa kama utaratibu ambao unamwonea mwanafunzi ambaye anahamu ya kujiendeleza kielimu lakini anakwama kwa sababu mfumo unaotumika siyo rafiki kwa mtahiniwa. Kwa mantiki hii, Wizara imedhamiria kufanya harmonization ya masuala ya alama katika mitihani ya Kidato cha Nne na Kidato cha Sita ili kupata muundo mmoja na ulio wazi kwa wadau wote wa elimu ya sekondari. Lakini pia serikali imedhamiria kuhakikisha tathmini za wanafunzi katika ngazi mbalimbali zinakwenda sambamba na matarajio ya mitaala inayotumika na ambayo inahuishwa mara kwa mara ili iendane na wakati na mahitaji ya elimu katika ngazi mbalimbali.
1
2.
DHANA YA MITIHANI NA ALAMA
Mitihani hutumika kwa madhumuni mbalimbali ikiwemo kupima endapo malengo ya kujifunza na kufundisha yamefikiwa na pia kubaini changamoto mbalimbali katika utoaji wa elimu katika ngazi husika. Kimsingi, mfumo wa mitihani ni jambo linalopangwa kwa kuangalia mambo mbalimbali ikiwemo hali halisi ya elimu katika ngazi husika. Mfumo unaweza kubadilika kulingana na elimu inavyoendelea kukua na mahitaji mbalimbali yanavyoendelea kujitokeza. Mtihani wowote lazima uwe na matokeo. Ili matokeo haya yapatikane, kila nchi imejiwekea utaratibu wa kuyapata matokeo hayo kulingana na malengo (objectives) ya mtihani husika. Kitaalamu, mtihani una uhusiano mkubwa sana na mitaala (curricula) na mihtasari yake na jinsi mitaala hiyo inavyofundishwa na wanafunzi kujifunza (curricula instruction or delivery). Mitihani pia huwa inafanyika katika muda maalum na kwa hivyo kuna: a) b) mitihani kwa ajili ya kupanga wanafunzi katika makundi (streams) kulingana na umahiri wao (placement assessment), mitihani ya kubaini kama ufundishaji unakwenda vizuri na changamoto zilizopo ili kuchukua hatua rekebu kadri mwanafunzi anavyoendelea kukua kielimu (diagnostic assessment), mitihani ya kubaini ukuaji wa mwanafunzi kielimu (formative assessment) na mitihani ya kumaliza elimu katika ngazi husika (summative assessment).
Inaendelea toleo lijalo

No comments:

Post a Comment