1. Punguza kutumia kilevi (pombe) badala yake ongeza kunywa chai, maji na juisi asilia ya matunda.
2. Punguza kula nyama (hasa nyama nyekundu za wanyama waliwao) badala yake ongeza ulaji wa mboga mboga za majani.
3. Punguza kutumia sukari nyingi au kula vyakula vyenye sukari nyingi badala yake ongeza ulaji wa matunda kwa wingi.
4. Punguza utumiaji wa chumvi nyingi au kula vyakula vyenye chumvi nyingi badala yake ongeza utumiaji wa siki (vinegar)
5. Punguza kuwa na wasiwasi au hofu ya aina yeyote ile badala yake pumzisha mwili wako kwa kuongeza ubora wa usingizi wako kwa kulala mahali safi, tulivu, penye hewa ya kutosha na kwa muda wa kutosha. (saa 6 mpaka 8)
6. Punguza kuwa na hasira kila wakati badala yake ongeza kutabasamu na kucheka kwa furaha kila unapofurahishwa.
No comments:
Post a Comment