Thursday, August 8, 2013

MUANDAMO WA MWEZI

Kwa nini waislam hatusherehekei mwezi mmoja?KAMA kuna wakati ambao umoja baina yao basi hakuna wakati muafaka kama huu tulio nao. Lakini kutafuta njia za kutufikisha katika umoja huo, sisi tumekuwa tukijishughulisha zaidi na mambo madogo madogo yenye ikhitilafu baina yetu, ambayo hayana faida yoyote kwetu, isipokuwa kutuongezea uhasama na utengano. Sala ya Idi ni Sunna lakini umoja wa Waislamu ni wajibu. Sisi tumeacha kulishughulikia lile jambo la wajibu, ambalo ni umoja wa Waislamu na tumeamua kutowafikiana katika kusali sala ya Idi siku moja bila ya kuwa na sababu yoyote ya msingi. Maswali ya lini tuanze kufunga Ramadhani na lini kufungua pamoja na swali la saumu ya Arafa yameleta ikhtilafu kubwa baina ya wanazuoni wetu. Kundi moja linadai kwa kuwa dunia ni moja na mwezi ni mmoja, basi mwezi ukiandama katika nchi yoyote ulimwenguni inabidi nchi nyingine zote zifuate. Itaendelea......

No comments:

Post a Comment